Serikali imefanikiwa kudhibiti vitendo vya ujangili hapa nchini kwa zaidi ya asilimia 50.
Hayo yameelezwa jana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati akizungumza na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Sarah Cooke ofisini kwake mjini Dodoma.
Mazungumzo hayo yalilenga kujadili mambo mbalimbali ikiwemo kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili katika sekta ya uhifadhi na maendeleo ya utalii.
Dk. Kigwangalla alisema katika kipindi cha miezi sita iliyopita hakuna mauaji mapya ya wanyamapori yaliyoripotiwa na kwamba nyara zinazokamatwa hivi sasa ikiwemo meno ya tembo na ngozi za wanyamapori ni masalia ya zamani.
Amesema mafanikio hayo yametokana na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali kudhibiti vitendo vya ujangili ikiwemo doria za mara kwa mara za kiitelijensia ambazo zimekuwa zikishirikisha vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama pamoja na raia wema.
Alisema Serikali itaendelea kudhibiti vitendo hivyo kwa kuimarisha ulinzi katika maeneo ya hifadhi nchini ikiwa ni pamoja na kuanzisha jeshi maalum la usimamizi wa Misitu na Wanyamapori, Sheria ya wanyamapori na za taasisi za uhifadhi zimeanza kufanyiwa marekebisho kuwezesha mabadiliko hayo.
Katika hatua nyingine Dk. Kigwangalla amemueleza balozi Cooke kuwa, Serikali kupitia Wizara yake inaendelea kuimarisha vivutio vya utalii hapa nchini kwa kupanua jeografia ya maeneo ya utalii sambamba na kuongeza vivutio ili kuongeza idadi ya watalii na mapato.
Amesema Serikali itajenga makumbusho ya Marais Wastaafu wa Tanzania mjini Dodoma pamoja kuanzisha makumbusho ya meno ya tembo katika miji ya Dar es Salaam, Arusha, Iringa na Dodoma.
Sambamba na hayo amesema Serikali itaanzisha mwezi maalum wa maadhimisho ya urithi wa Mtanzania ambao utafanyika mwezi Septemba kila mwaka pamoja na kuendeleza utalii wa mikutano.
Amesema Serikali pia itaanzisha Mamlaka ya Usimamizi na Uendelezaji wa Fukwe nchini ili kuimarisha utalii wa fukwe pamoja na kutambua barabara iliyokuwa ikitumika katika biashara ya utumwa wakati wa ukoloni ili iweze kutumika kiutalii.
Akizungumzia migogoro ya mipaka iliyopo baina ya wananchi na maeneo ya hifadhi, Dk. Kigwangalla alisema Serikali itatatua migogoro hiyo kwa kushirikisha wananchi sambamba na kuwasaidia kutatua changamoto za msingi ambazo ni kuimarisha maeneo ya malisho ya mifugo, upatikanaji wa maji kwa ajili ya wananchi na mifugo, mpango bora wa matumizi ya ardhi na uendelezaji wa kilimo na ufugaji.
Kwa upande wake balozi Cooke alisema nchi yake itaendelea kuimarisha ushirikiano inaoutoa kwa Serikali ya Tanzania katika kudhibiti mtandao wa uhalifu wa madawa ya kulevya, rushwa na ujangili.
Alisema kwa sasa watalii zaidi ya 75,000 wa Uingereza hutembelea Tanzania kila mwaka na wengine wamewekeza katika sekta utalii hapa nchini, hivyo akaiomba Serikali kurekebisha baadhi ya changamoto chache zilizopo katika sekta hiyo kwenye mtiririko wa kodi.



Related
Published by Mbilinyi-Wildlife
Conservation has always been a major part of my life. Growing up I revered leaders like famous oceanographer Jacques Cousteau and conservationist Jane Goodall, and I dreamed of becoming a swayful wildlife conservationist one day. Some of my fondest memories are of exploring the Amani forests with my college's friend, learning about both the awesome power of nature the threats to its well being.
I ultimately pursued a career in wildlife management at college of African wildlife management -Mweka and my friends too become a conservationists. Together, we founded Saviours of Wildlife with our slogan that Who pays for wildlife and who benefits?.
I recognize there are many conservation organizations doing incredible work on behalf of our planet and the many species who call it home.
I wanted to create an organization that complemented and collaborated with these organizations, so we chose to focus on protecting lesser-known endangered species.
My speech
If there’s one thing we know about life on Earth, it is that all of our diverse animals, plants, soil structures and waterways are interconnected in complex ways, many of which we cannot fully understand. In order to maintain ecological balance, we need to focus on all of the puzzle pieces–and this is becoming harder to do as we lose more and more species to climate change and human activity.
Saviors of wildlife focuses on lesser-known species because they are our early-warning signals for larger issues facing the ecosystem. For example, amphibians have a tremendous impact on their environment. They are not the face of environmental conservation in the same way as elephants,rhinoceros or gorillas, but because of their size and genetic makeup, these creatures are much more sensitive to climate change.
For example, saviour of wildlife is working to save amphibians, reptiles but also supporting efforts of conserving big wildlife like Rhino, giraffe and elephants through conservation education and capacity building to wildlife practititoners.
Saviours of wildlife is also working to save the world’s most endangered marine mammals. Only about 30% are left in the wild due to them becoming entangled in gill nets set for illegal fishing activities.The marine creatures are the most endangered Species.
Our planet is facing a biodiversity crisis. Last month , I was fortunate to share comment with Jane Goodall to discuss this critical issue. She reminded the word that she spoke to me 5 years ago “don’t forget, every single one of you makes a difference every single day.”
As we sit on the brink of losing thousands of more species, throwing our future into jeopardy, I am now asking you to make smart decisions .Please join us in reversing this crisis and making our collective future more secure contact
Brighton Mbilinyi, saviours of wildlife,college of African wildlife management.
brightonfrancis91@gmail.com +255756 525739
View all posts by Mbilinyi-Wildlife